Wafuasi mbalimbali Misri
Watu wasiojulikana wamewaua waandamanaji 11 waliopiga kambi
nje ya makao makuu ya Watawala wa Kijeshi Mjini Cairo,Misri.
Maafisa wanasema watu hao walianza kuwashambulia
kwa mawe, mabomu na risasi waandamanaji hao ambao pia walijibu mashambulizi
hayo. Wanajeshi pamoja na polisi wamezika makabiliano hayo, lakini baada ya saa
sita za vurugu .
Kufuatia tukio hilo wagombea wawili wakuu wa Urais
wamesimamisha kampeini zao kulalamikia mauaji hayo.
Abdul Moneim Aboul Fotouh,mgombea wa kujitegemea pamoja na kiongozi wa chama Freedom and Justice Party ambacho kinaungwa mkono na Muslim Brotherhood Mohammed Mursi wamelaani maafisa wa usalama kwa kuchelewa kuzuia fujo hizo.
Aidha chama cha FJP na kile cha Salafist Nour ambavyo vina wabunge wengi vimesusia mkutano na Baraza tawala la kijeshi{Scaf}.
Maandamano kulalamikia utawala wa kijeshi yameendelea tangu jeshi lichukue madaraka baada ya kuondolewa kwa Rais Hosni Mubarak Februari mwaka 2011.
Watawala wa Kijeshi wamelaumiwa kwa kuwakandamiza wapinzani na kuwaua waandamanaji pamoja na kuzima mashirka ya kiraia.
Watawala wa kijeshi hata hivyo wameahidi kuyakabidhi madaraka kwa raia mwishoni mwa mwezi Juni baada ya kufanyika uchaguzi wa Urais ambao wanasema utakuwa huru na haki
Abdul Moneim Aboul Fotouh,mgombea wa kujitegemea pamoja na kiongozi wa chama Freedom and Justice Party ambacho kinaungwa mkono na Muslim Brotherhood Mohammed Mursi wamelaani maafisa wa usalama kwa kuchelewa kuzuia fujo hizo.
Aidha chama cha FJP na kile cha Salafist Nour ambavyo vina wabunge wengi vimesusia mkutano na Baraza tawala la kijeshi{Scaf}.
Maandamano kulalamikia utawala wa kijeshi yameendelea tangu jeshi lichukue madaraka baada ya kuondolewa kwa Rais Hosni Mubarak Februari mwaka 2011.
Watawala wa Kijeshi wamelaumiwa kwa kuwakandamiza wapinzani na kuwaua waandamanaji pamoja na kuzima mashirka ya kiraia.
Watawala wa kijeshi hata hivyo wameahidi kuyakabidhi madaraka kwa raia mwishoni mwa mwezi Juni baada ya kufanyika uchaguzi wa Urais ambao wanasema utakuwa huru na haki
Mwanaharakati wa Uchina Chen Guangcheng
Mwanaharakati wa Uchina Chen Guangcheng amesema kuwa
anahofia maisha yake na kwamba anataka kuondoka. Amesema hayo saa chache baada
ya kuondoka hifadhi katika ubalozi wa Marekani.
Bw Chen amesema aliondoka kwenye ubalozi huo baada ya
maafisa wa Uchina kutishia wanachama wa familia yake.
Lakini Marekani imesema haina habari zozote kuhusu vitisho
hivyo na kwamba mwanaharakati huyo hakuomba hifadhi wakati wowote.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, yuko mjini Beijing kwa mazungumzo ya kibiashara na usalama na maafisa wa Uchina.
Awali, Bibi Clinton aliunga mkono Bwana Chen, ambaye amekuwa katika kifungo cha nyumbani kwa takriban miaka miwili.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, yuko mjini Beijing kwa mazungumzo ya kibiashara na usalama na maafisa wa Uchina.
Awali, Bibi Clinton aliunga mkono Bwana Chen, ambaye amekuwa katika kifungo cha nyumbani kwa takriban miaka miwili.
haki za binadamu
Lakini wakati mazungumzo yalipoanza Bibi Clinton hakumtaja kwa jina.''Marakeni inaamini kuwa hakuna nchi ina haki ya kumyima mtu haki ambayo ni haki ya kila binadamu- au kuadhibu mtu ambaye anatumia haki hizo. Bibi Clinton alisema.
Hapo Jumatano maafisa wa Uchina walishutumu Marekani kwa kuingilia maswala ya ndani ya nchi yao na kutaka Marekani iombe msamaha kwa kumhifadhi Bwana Chen katika ubalozi wao.
Mkutano unaofanyika Uchina ulitarajiwa kuzungumzia Syria na Korea ya kaskazini lakini imeghubikwa na mzozo wa kidplomasia juu ya Bwana Chen.
Bwana Chen amekuwa katika ubalozi wa Marekani kwa wiki moja baada ya kutoroka kutoka kifungo cha nyumbani katika kijiji chake kilichoko katika mkoa wa Mashariki cha Shandong
SHARE TO
kujishindia mamilioni bonyeza hapo chini, ==>>
International reporting trip.27 year old Missouri woman named Evelyn was recently featured on TLC's "My Strange Addiction", where she revealed that she's addicted to drinking air-freshner. According to Evelyn, she drinks 20 cans of air freshner a week and sprays up to 50 times daily.
Post a Comment